Roberto Di Matteo, amezaliwa 29 Mei 1970. Ni mwanasoka wa
zamani kutoka nchini Itali na ndiye kocha wa mpito wa timu ya Chelsea kwa msimu ulioishia mwaka 2012.
Kipindi anacheza soka, alicheza kama kiungo katika klabu ya Uswiss Schaffhausen, Zurich
na Aarau kabla ya kujiunga na klabu ya Lazio na Chelsea ya Uingereza.
Aliichezea timu ya Italy
mara 34, akifunga jumla ya magoli mawili, alicheza kwenye kombe la Euro mwaka
1996 na Kombe la dunia 1998.
Alistaafu kama mchezaji Februari 2002 akiwa na umri wa miaka
31, baada ya kuandamwa na matatizo ya majeruhi. Tangu hapo amekuwa akiziongoza
Amezaliwa Uswis, Wazazi wake ni raia
wa Itali kutoka mji wa Paglieta, Abruzzo, Di Matteo alinza safari yake ya soka
kwa kuichezea klabu ya Uswis Schaffhausen, kabla ya kujiunga na klabu ya Aarau
mwaka 1991. Alitwaa ubwinga wa Nationalliga A, akiwa na klabu ya Aaru mwaka
1993.Ligi hiyo ikiwa ni ligi ya 14 kwa ubora barani Ulaya kwa mujibu wa UEFA.
Katika kipindi hicho hicho alifanikiwa kujinyakulia tuzo ya uchezaji bora wa
mwaka, Mwaka 1993 alisaini uhamisho bure
kipindi cha majira ya joto na kuelekea kuelekea klabu ya Lazio. Di
Matteo alitokea kuchezea timu ya Lazio mara kwa mara na ndipo alipoanza kutokea kwenye kikosi cha Timu yake ya Taifa ya Itali
kipindi anachezea klabu yake ya jijini Roma.
Hata hivyo mfarakano baina yake na
kocha wake Zdeněk Zeman, baada ya kosa la kiulinzi
lililopelekea kufungwa na timu ya Internazionale, ulimaliza safari yake na
timu ya Lazio, matokeo yake akasainiwa na Ruud Gullit wa Klabu ya Uingereza kwa
dau lilioweka rekodi ya £ 4.9 milioni.
Di Matteo alifunga goli la ushindi dhidi ya Middlesbrough
katika mchezo wa nyumbani akiwa na klabu yake ya Chelsea katika mchezo wake wa
kwanza.Uwezo wake wa kutoa pasi zenye uwezo wa hali ya juu na mashuti ya mbali
yenye usahihi, ulimfanya awe ni mmoja wa wachezaji wenye uwezo na msukumo wa
hali ya juu wa klabu yake ya Chelsea mwishoni mwa miaka ya tisini. Alichangia
magoli tisa. Ikiwemo misaada ya umbali mrefu dhidi ya Tottenham Hotspur na
Msimu uliofata Di Matteo aliendelea kudhihirisha thamani
yake kwa timu yake, kwa kupachika magoli kumi na kutoa misaada ya hapa na pale, na
Katika msimu wa mwaka 1999-2000 Di Matteo alitolewa kikosini
kutokana na majeraha ila aliridu mwishoni mwa msimu na kufunga magoli muhimu,
likiwemo goli lake la tatu la ushindi ndani ya Wembley kwa mara nyingine katika
kombe la FA, katika mchezo mgumu Di Matteo alitumia nafasi vizuri iliotokana na
kosa lililofanywa na kipa wa Aston Villa David James katika dakika ya 71 na
kujipatia goli la ushindi, na kuwazawadia Chelsea kwa mara nne katika kipindi
cha miaka mitatu. Hii ilimfanya Di Matteo Aseme” ni aibu kuona wanauteketeza ,
umekuwa ni uwanja wenye bahati sana
kwangu”
Mwanzoni mwa msimu wa mwaka 2000 na 2001, alijikuta
akivunjika mguu mara tatu katika kombe la UEFA dhidi ya St gallen klabu ya
Uswisi na kutocheza kwa miezi 18 iliofata. Februari 2002 alitupilia mbali
matumaini ya kurudi kucheza akitoka kwenye majeruhi aliyoyapata na kustaafu
katika umri wa miaka 31.
“kama shukrani ya mchango kutoka kwa kiungo uliochangia
mabadiliko ya klabu” kocha wa kipindi hicho Claudio Ranieri alimpa heshima ya
kukiongoza kikosi cha Chelsea katika fainali za kombe la FA 2002, ambapo
ilipoteza dhidi ya Arsenal kwa 2-0.
Di Matteo alichaguliwa kama
mchezaji wa Kihistoria wa klabu ya Chelsea. Katika miaka sita alipokuwa Chelsea aliichezea Chelsea
mara 175 nakushinda magoli 26, hakuwahi kupoteza uwanjani Old Trafford
Kimataifa
Di Matteo alitokea katika kikosi cha timu ya Itali kwa mara
ya kwanza 16 Novemba 1994 ndani ya uwanja wa Stadio La Favorita, Palermo, Sicily. Aliingia uwanjani
dakika ya 55 kama mbadala wa Demetro Albertinias, Itali ilipoteza 2-1 dhidi ya
Croatia katika mechi za kufuzu Euro 1996.Alianza mwanzoni mwa mchezo katika
mchezo wake wa pili katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Uturuki tarehe 21
Desemba 1994 katika uwanja wa Stadio
Adriatico ndani Pescara.
Ambapo ilishinda 3-1. Aliendelea kucheza timu yake ya Itali katika ngazi ya
makundi 1996 dhidi ya Urusi na Ujerumani
Goli lake la kwanza alifunga kwenye mchezo wake wa 23 akiwa
na timu yake ya taifa, katika michezo ya kufuzu kombe la Dunia la mwaka 1998
mnamo 30 April 1997, Itali ilishinda 3-0 dhidi ya Poland.Di matteo.DI Matteo
alifunga goli moja la ziada, dhidi ya Slovakia Januari 1998. Alikuwemo kwenye
kikosi cha kombe la dunia la mwaka 1998 na kuchezea michezo miwili ya ngazi ya
makundi dhidi ya Chile na Cameroon . Mechi
dhidi ya Cameroon Montpeller ndiyo uliokuwa mchezo wake wa mwisho kuichezea
timu yake ya Itali.
Akiwa kama Kocha wa Chelsea
Akiwa kama Kocha wa Chelsea
Baada ya kushindwa kufanikiwa kuwa
meneja wa timu ya Birmingham
City . Di Matteo
aliteuliwa kuwa kocha msaidizi wa André Villas-Boas (kocha mpya wa Chelsea 29
Juni 2011).
Baada ya kufukuzwa kazi kocha André Villas-Boas, Di Matteo alipewa madaraka
ya mpito na kuiongoza timu ya Chelsea kuanzia
March 2012.Aliendelea kutambulika kama kocha
wa mpito kwa mujibu wa klabu ya Chelsea. Alianza kupata mafanikio ya moja kwa
moja mara tuu baada ya kupewa timu, alishinda dhidi ya Birmingham
City , katika mzunguko wa tano wa kombe
la FA, Stoke city katika ligi ya Uingereza na Napoli katika mzunguko wa 16
kombe la Klabu bingwa UEFA nakushinda 4-1 baada ya mechi ya kwanza Chelsea kupoteza 3-1, walipokuwa
chini ya uongozi wa André Villas-Boas
Di Matteo alishinda dhidi ya
Tottenham kwenye nusu fainali za kombe la FA na Dhidi ya Benfica kwenye robo
fainali ya UEFA, tarehe 24 April aliipatishia
Chelsea ushindi dhidi ya Barceloma kwenye nusufainali kwa jumla ushindi wa 3-2
nyumbani na ugenini, na kuwa toa
barcelona waliokuwa wakitetea ubingwa wa klabu bingwa UEFA, Mei 5 Chelsea
ilishinda dhidi ya Liverpool 2-1 kwenye mchezo wa fainali wa kombe la FA ndani ya
uwanja wa wembley.
19 Mei Di Matteo aliingoza Chelsea
nakushindaUEFA kwa kuishinda klabu ya Ujerumani Bayern Munich,
ushindi mnono ulipatikana kwa penati, na kuifanya Chelsea kushinda kombe la
UEFA kwa mara ya kwanza na kuifanya ifuzu katika msimu wa klabu bingwa ulaya wa
2012-2013, baada ya kuto maliza miongoni mwa timu nne ambazo zingesonga mbele,
hii ikapelekea pelekea kutolewa kwa wapinzani wao wa jijini London Tottenham Hotspur kutofuzu katika
kinyanganyoro hicho cha UEFA.
Maisha
yake ya Kifamilia

No comments:
Post a Comment