Toleo la mwaka 2011 May 31
Mafanikio
ya mwanamichezo Tiger Woods, imekuwa ikidorora kwa kipindi cha miaka miwili
iliopita. Wadhamini wakubwa
Biashara
yake ya kudizain viwanja vya golf nayo iliporomoka kifaida kutoka na mporomoko
wa hali ya uchumi duniani.Na nuksi ya muendelezo wa kutoshinda kwenye
vinyanganyiro vya mashindano ya golf kwa
kipindi cha miezi 20 na ushee, imepelekea gwiji huyo aliyekuwa mwanamichezo
namba moja katika michezo ya golf kuwa wa 13 duniani, na mapato yake ya kipungua kwa dola
milioni 50, kwa kipindi cha miaka 2 miwili iliyopita.
Pamoja
na yote hayo Tiger Woods bado ndiye mwanamichezo namba moja ulimwenguni kwa
kulipwa pesa nyingi, na hakuna anayemkaribia kwa karibu, Akipata dola za kimarekani
milioni 75 kwa kipindi cha miezi 12 iliopita, akimuacha kwa mbali sana Kobe Bryant
aliyejitengezea dola milioni 53 za kimarekani katika msimu huo huo.
Mafanikio
yake kwa zaidi ya asilimia hamsini yametokana na wadau wake wa muda mrefu
Kampuni ya Nike na Electronic Arts, ambao wote hawa waliingia naye mkataba
kuanzia mnamo mwaka 1998 akipokuwa rasmi mwanamichezo professional,
Kwa mara nyingine tena wanamichezo wa kike, wakiwa nyuma katika
takwimu hizi za wanamichezo wanaolipwa zaidi duniani.Mcheza Tennis Mara
Sharapova ndiye mwanamke pekee aliyeweza kupenya katika orodha ya wanamichezo
50 wanaolipwa zaidi duniani, ni wa 29 akijipatia dola milioni 24.2, kwa kiasi
kikubwa kutoka kwa wadau wake kama Nike.
HABARI HII NI TOLEO LA MWAKA JANA TAREHE 31 MAY 2011, KWA MUJIBU WA
TAKWIMU ZA FORBES


No comments:
Post a Comment