Friday, 15 June 2012

SITE UNDER REVIEW STAY TUNED/MTANDAO UNAFANYIWA MAPITIO ENDELEA KUFATILIA

Wednesday, 6 June 2012

Proff Jize akipafom kwenye show : DAR LIVE


Picha kwa Hisani ya National Geographic Channel

Child Portrait kwa hisani ya National Geographic Channel


Arctic skuas, also called parasitic jaegers, have a well-earned reputation as avian pirates, stealing much of their food from other birds.

Mabilionea Vijana Duniani


Mabilionea wanne vijana wanahusika moja kwa moja na facebook, wawili ni watoto wa aliyekuwa Waziri mkuu wa Lebanon Hayati Rafic Hariri, na mmoja ni mwananke. Wafuatao ni mabilionea  vijana kwa mujibu wa mtandao wa peekyou.com

1. Mark Zuckerberg
Mark Zuckerberg ambaye sasa anaumri wa miaka 28, alizindua facebook kwenye bweni lake kipindi anasoma chuo na amekuwa huku akizungukwa na wafanyabiashara wenye mafanikio makubwa duniani. Utajiri umeongezeka kwa kasi baada ya kuiorodhesha facebook kwenye soko la hisa, anathamani ya dola bilioni 15 kwa mujibu wa takwimu. Ndiye anaengoza katika orodha ya mabilionea vijana.

2. Scott Duncan
Sasa akikaribia umri wa umri wa miaka 30, amejipatia utajri wake kwa kuridhi mali kutoka kwa marehemu mzee wake, ambaye alianzisha kampuni ya Energy. Anasadikika kuwa na thamani ya dola bilioni 4 za kimarekani

3. Dustin Moskovitz
Moskovitz alifahamina na Mark tangu wapo chuoni, alifanya kazi Facebook kipindi  cha awali cha ukuaji wa kampuni ya facebook, Hivi karibuni ameamua kujihusisha na michakato mingine ikiwemo na shuhuli za misaada, kwa mujibu wa forbes anathamani ya dola bilioni 3.5



4.Sean Parker
Muanzilishi wa Kampuni ya Napster na raisi wa kwanza wa Facebook anathamani ya zaidi dola bilioni mbili. Parker mwenye umri wa miaka 32, amekuwa mshauri mkuu wa zuckerberg na ndiye anayefahamika zaidi kwa kumshauri Mark kubadilisha jina la kampuni ya facebook kutoka kwenye kuitwa “ the facebook” hadi “facebook”. Na ndiye aliyekuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kuwekeza kwenye mtandao wa muziki wa Spotify

5. Eduardo Saverin
Ni mwanzilishi mwenza wa facebook ambaye sasa anamakadirio wa utajiri wenye thamani ya dola bilioni 2, ila ilimlazimu kupigania hadhi yake hiyo, aliishitaki kampuni ya facebook, yalifanyika maelewano nje ya mahakama. Kama ilivyo wasilishwa kwenye filamu ya "The social Network", Saverin mwenye umri wa miaka 30, amekulia kwenye familia ya kitajiri anafahamika kama mpenda kula  bata.

Wengineo ni pamoja na ...
Fahdi Hariri
Robert Pera
Ayman Hariri
Yang Huiyan
Albert Von Thurn Und Taxis

Tweet kutoka kampuni ya Asus iliozua Utata


 Ni ujumbe wa twita, uliozua mijadala kwenye mitandao ya intaneti kwa kushutumiwa kuwa unamdhalilisha mwanamke. Kampuni ya Electronics Asus iliufuta ujumbe wake huo ulioambatanishwa na picha inayomuonyesha mwanamke akielezea bidhaa mpya ya kampuni hiyo mara tu baada malalamiko kuanza.
Ni picha iliopigwa kwa kuuchukua upande wa nyuma ya mwili wa mrembo huyo ikiambatana na ujumbe unaosema “ picha ya nyuma ni nzuri sana,  kama ilivyo Transformer AIO”
Posti hiyo ilipotea kwa haraka sana, ila walichelewa kwani ilishadakwa na watu kuanza kuichangia na wenzao, na kusambaa kwa kasi kwenye mitandao mingine na  malalamiko na shutuma kuanza kuelekezwa kwa kampuni hiyo.hata hivyo kampuni ya Asus iliomba radhi kwa tukio lake hilo, na kuahidi kuchukua hatua ambazo zitahakikisha kosa hilo halitojitokeza tena
Utamadani wa kuwatumia wanawake warembo kwenye maonyesho ya bidhaa, umekuwa ni utaratibu wa wakawaida kwa makampuni ya elektroniki duniani. Ila tahadhari itumike, na kwa uangalifu wa karibu zaidi, aliongezea Bi susan Friedmann mtaalamu wa maswala ya ya biashara kwa kusema “ nilazima uzingatie unapofanya maonyesho kama haya, kinachoweza kukufunga Paducah yaweza kuwa sawa na Tokyo”

Kampuni ya Kidachi yaanzisha Makazi sayari ya Mars ifikapo mwaka 2023


Rover
Inaonekana kama ni nadharia ya kisayansi ambayo daima haiwezekani, kuwa halisi, kampunni ya Mars one ya Kidachi, imetamba kuwa wazo hilo ni halisia na mchakato mzima wa ujenzi wa makazi hayo utakamilika ifikapo mwaka 2023.
Kampuni hiyo binafsi inayo mpango madhubuti kilichobakia sasa ni Pesa ya kutosha kuufadhili huo mradi , vifaa na wana anga ambao wapo tayari kufanya safari ya moja kwa moja  kuelekea sayari ya mars pasi na kurudi kwenye sayari ya duniani. Ambapo na watategemewa kuishi huko kwa kipindi chote cha maisha yao
Mpangilio mzima ni kuanza kwa, kupeleka vifaa vya uchunguzi na usafirishaji(rovers), ambavyo vitakamilisha jukumu la kuteua eneo zuri  la ujenzi na kuanza kujenga makazi. Ifikapo mwaka 2022 kundi la kwanza litaelekea kwenye sayari hiyo, safari inayotegemewa kuchukua miezi saba, kuweka kambi katika makazi yao mapya.lengo likiwa ni kuanza maisha mapya na kuishi huko kwa kipindi chote cha maisha yao, kisha kila baada ya miaka miwili kundi jingine la watu litakuwa likienda kwenye makazi hayo.
Ikiwa inafananishwa na Big Brother, tayari mradi huo umepata baraka za kutosha kutoka kwa wadau wanaojihusisha na mambo ya anga kutoka nchi  mbali mbali duniani. Ambao watachangia vifaa vya ujenzi na kutoa mchango wa kitaalama pale itapohitajika. Ni mradi binafsi ambao hautegemeai pesa za walipa kodi kwa hiyo haitegemewi kutokea mifarakano yoyote au kusitishwa kwa  sababu za kisiasa au hila za wanasiasa.

Muazilishi wa mradi huo ndugu Bas Lansdorp, anatazamia kutumia mbinu ya kisasa. Ujenzi wa makazi hayo utakuwa ukirushwa hewani moja kwa moja na kutoa nafasi ya kila mmoja kuweza kuushuhudia ukiendelea.
Video ya Mars one imeshapata zaidi ya watazamaji 232, 000 tangu iliporushwa kwenye youtube,com
Tayari baadhi ya wanasayansi waliobobea wameanza kuonesha shaka juu ya mradi huo, kwamba upo kinadharia zaidi.
Kwa mujibu wa mtandao Mars one kuanzia mwakani wataanza uteuzi wa wana anga watakaoshiriki kwenye mradi huo

PROMETHEUS 3D IN CINEMAS