Kampuni ya
google imekuwa ikiendeleza upinzani wake kwa kampuni ya microsoft kwa kitendo
chake cha hivi karibuni kuinunua kampuni inayojishuhulisha na utengenezaji wa
programu ya QUICKOFFICE,
Quickoffice
ni programu inayofanya kazi kwenye simu,na komputa za mikononi lengo
Hii itaongeza
upinzani kwa kampuni ya microsoft kwa kuviwezesha vifaa kama
ipad na vingine ambavyo microsoft haija unda nakala ya programu ya microsoft
office. kuweza kufanya kazi kwenye vifaa hivi na kuvipa uwezo wa kufungua mafaili yaliyo katika mfumo huo.
Mkurugenzi
wa kampuni ya microsoft amezikosoa programu zinazotengezwa na Google kwa kudai
kuwa hazikidhi mahitaji ya watumiaji kwa ukamilifu.
Ingawa mapato
ya kampuni ya quickoffice yanatokana na matangazo, programu hiyo imekuwa
ikitumia na ikifanya kazi katika vifaa takribani milioni 400, ambapo kila
programu inauzwa kati ya dola 15 hadi 20. na inawatoza wateja wake pesa kidogo
kwa wale watakaohitaji programu hizo kuwa na uwezo wa ziada kama
kuandika au kurekebisha.
Quikoffice
yenye makao yake makuu nchini marekani katika jimbo la Texas linawafanyakazi 400 na ipo chini ya Alan
Masarek ambaye aliianzisha kampuni hiyo miaka kumi iliopita,
Ambapo
google yenye makao makuu yake nchini marekani pia, mwishoni mwa mwezi wa machi
lilikuwa na jumla ya wafanyakazi 33 000, na ilijiongezea wafanyakazi 20, 000 baada ya kukamilisha
ununuzi wa kampuni ya Motorola Mobility kwa dola za kimarekani bilioni 12,5

No comments:
Post a Comment