Monday, 4 June 2012

Wanamichezo Mashuhuri wanaolipwa zaidi Ulimwenguni


Wanamichezo mashuhuri wenye mvuto wa kibiashara zaidi duniani, ambao wamekuwa miongoni mwa orodha ya watu 100 mashuhuri duniani, orodha yao imesambaa kutoka kwenye  michezo tofauti tofauti duniani.wanamichezo 17 wamefuzu kuwemo katika orodha ya watu mashuhuri 100( wanaume wakiwa 14 na wanawake 3) wote hawa wakitokea katika michezo saba tofauti na wamezaliwa katika nchi 9 tofauti tofauti.

Akiungoza msafara huu ni Tiger woods, ambaye ni wa 12 kutoka wa 6 kwa mwaka 2011.Mapato ya Tiger woods yameporomoka kutoka dola milioni 75 kwa mwaka jana hadi dola milioni 58 kwa mwaka huu, ikichangiwa na kujiondoa kwa wadhamini wake wakubwa kama Gillete, ila bado ameendelea kushikilia kiwango cha juu cha kulipwa kama mwanamichezo duniani, uwiano wa umaarufu wake umewazidi wanamichezo, wote jina lake likitajwa sana kwenye vyombo vya habari hasa runinga na redio, akiwa wa sita miongoni kwa watu mashuhuri 100 kwa ujumla.

Wanasoka waongoza miongoni kwa wanamichezo wa kiume, ikiwa ni  mchezo pekee wenye wanamichezo watatu wakiume wakitokea katika aina moja ya mchezo, ni David Beckham(32), Christiano Ronaldo( 44) na Lionel Messi(50).Ukiachilia mbali  kiwango kikubwa cha mapato yao, wote watatu wamekuwa na wafuasi wengi katika mitandao ya kijamii,  wote kwa ujumla wakiwa na wafuasi facebook milioni 95. Kitendo hicho kimekuwa kikiwaongezea thamani hasa kimatangazo kwa wadhamini kama Nike(Ronaldo) na Adidas(beckham, Messi)


LI Na
Wanamichezo wakike watatu miongoni mwa watu mashuhuri 100 duniani wametokea katika aina moja ya mchezo , Maria sharapova kwa mara nyingine akiongoza kutoka dola millioni 24.6 hadi dola milioni 26 kwa kipindi cha miezi 12 iliopita, ambapo Serena Williams(76) akiwa na mvuto wa aina yake katika medani ya tennis, na hatimaye mwanatenis Li Na(88) kutoka china ni mgeni katika dira hili, mwaka jana kwenye Grand Slam akishinda taji la French Open.Aliendeleza mafanikio nje ya viwanja vya tennis akijipatia mikataba minono iliompa dola za kimarejani milioni 7 kutoka Mercedes na Samsung baada ya ushindi wake huo wa Jijini paris. Watu mashuhuri wageni wenza wa Li Na ni pamoja na Rihanna na Kim Kardashian

Wana NBA wameporomoka kwa namna Fulani kutokana na kuwa nje kimechezo kwa muda wa miezi mitano, ikiwagharamu asilimia 20 ya mapato yao,  ambapo msimu ulifupishwa hadi kuwa na michezo 66 kwa kila timu. Matokeo haya yamewapeleka Dwayne Wade na Dwight Howard kutoka kuwepo katika orodha ya mwaka huu, wakiungana na wenzao Charlie sheen na Jay leno



Kufanikisha kuwepo katika orodha ya watu mashuhuri 100 miongoni mwa wanamichezo inahitaji umaarufu wa hali ya juu na Mkwanja Mnene.Mwana Michezo bora wa Super Bowl kwa kipindi cha misimu mitatu Bingwa Tom Brady ndiye mwenye mapato madogo zaidi kulinganisha na wenzake katika msimu wa miezi 12 ilipiopita miongoni mwa wanaume kwa kujipatia dola milioni 27.
Je ni wanamichezo gani wanaotegemewa kuwemo katika orodha ijayo? Ni mwana kikapu Kevin Durant ambaye amekuwa akiongoza kwa mfululizo katika ufungaji kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo pamoja na |Derrick Roses ambaye ongezo la mkataba wake kwa Timu yake ya Chicago Bulls(milioni $95 kwa kipind cha miaka 5) na Adidas(milioni $ 185 kwa zaidi ya miaka 13)




No comments:

Post a Comment