![]() |
| Rover |
Kampuni hiyo binafsi inayo mpango madhubuti kilichobakia sasa ni Pesa
ya kutosha kuufadhili huo mradi , vifaa na wana anga ambao wapo tayari kufanya
safari ya moja kwa moja kuelekea sayari
ya mars pasi na kurudi kwenye sayari ya duniani. Ambapo na watategemewa kuishi huko kwa kipindi chote cha maisha yao
Mpangilio mzima ni kuanza kwa, kupeleka vifaa vya uchunguzi na usafirishaji(rovers),
ambavyo vitakamilisha jukumu la kuteua eneo zuri la ujenzi na kuanza kujenga makazi. Ifikapo
mwaka 2022 kundi la kwanza litaelekea kwenye sayari hiyo, safari inayotegemewa
kuchukua miezi saba, kuweka kambi katika makazi yao
mapya.lengo likiwa ni kuanza maisha mapya na kuishi huko kwa kipindi chote cha
maisha yao ,
kisha kila baada ya miaka miwili kundi jingine la watu litakuwa likienda kwenye
makazi hayo.
Ikiwa inafananishwa na Big Brother, tayari mradi
huo umepata baraka za kutosha kutoka kwa wadau wanaojihusisha na mambo ya anga
kutoka nchi mbali mbali duniani. Ambao
watachangia vifaa vya ujenzi na kutoa mchango wa kitaalama pale itapohitajika.
Ni mradi binafsi ambao hautegemeai pesa za walipa kodi kwa hiyo haitegemewi kutokea
mifarakano yoyote au kusitishwa kwa
sababu za kisiasa au hila za wanasiasa.
Muazilishi wa mradi huo ndugu Bas Lansdorp,
anatazamia kutumia mbinu ya kisasa. Ujenzi wa makazi hayo utakuwa ukirushwa
hewani moja kwa moja na kutoa nafasi ya kila mmoja kuweza kuushuhudia
ukiendelea.
Video ya Mars one imeshapata zaidi ya watazamaji 232, 000 tangu iliporushwa
kwenye youtube,com
Tayari baadhi ya wanasayansi waliobobea wameanza kuonesha
shaka juu ya mradi huo, kwamba upo kinadharia zaidi.
Kwa mujibu wa mtandao Mars one kuanzia mwakani
wataanza uteuzi wa wana anga watakaoshiriki kwenye mradi huo

No comments:
Post a Comment