Mabilionea wanne vijana wanahusika moja
kwa moja na facebook, wawili ni watoto wa aliyekuwa Waziri mkuu wa Lebanon
Hayati Rafic Hariri, na mmoja ni mwananke. Wafuatao ni mabilionea vijana
kwa mujibu wa mtandao wa peekyou.com
1. Mark Zuckerberg
Mark Zuckerberg ambaye sasa anaumri wa
miaka 28, alizindua facebook kwenye bweni lake kipindi
anasoma chuo na amekuwa huku akizungukwa na wafanyabiashara wenye mafanikio makubwa
duniani. Utajiri umeongezeka kwa kasi baada ya kuiorodhesha facebook
kwenye soko la hisa, anathamani ya dola bilioni 15 kwa mujibu wa takwimu. Ndiye anaengoza
katika orodha ya mabilionea vijana.
2. Scott Duncan
Sasa akikaribia umri wa umri wa miaka 30, amejipatia utajri
wake kwa kuridhi mali
kutoka kwa marehemu mzee wake, ambaye alianzisha kampuni ya Energy. Anasadikika
kuwa na thamani ya dola bilioni 4 za kimarekani
Moskovitz alifahamina na Mark tangu wapo chuoni, alifanya kazi Facebook kipindi cha awali cha ukuaji wa kampuni ya facebook, Hivi karibuni ameamua
kujihusisha na michakato mingine ikiwemo na shuhuli za misaada, kwa mujibu wa
forbes anathamani ya dola bilioni 3.5
4.Sean Parker
Muanzilishi wa Kampuni ya Napster na
raisi wa kwanza wa Facebook anathamani ya zaidi dola bilioni mbili. Parker mwenye
umri wa miaka 32, amekuwa mshauri mkuu wa zuckerberg na ndiye anayefahamika
zaidi kwa kumshauri Mark kubadilisha jina la kampuni ya facebook kutoka kwenye
kuitwa “ the facebook” hadi “facebook”. Na ndiye aliyekuwa miongoni mwa watu wa
mwanzo kuwekeza kwenye mtandao wa muziki wa Spotify
5. Eduardo Saverin
Ni mwanzilishi mwenza wa facebook
ambaye sasa anamakadirio wa utajiri wenye thamani ya dola bilioni 2, ila
ilimlazimu kupigania hadhi yake hiyo, aliishitaki kampuni ya
facebook, yalifanyika maelewano nje ya mahakama. Kama
ilivyo wasilishwa kwenye filamu ya "The social Network", Saverin mwenye umri wa
miaka 30, amekulia kwenye familia ya kitajiri anafahamika kama mpenda kula bata.
Wengineo ni
pamoja na ...
Fahdi Hariri
Robert Pera
Ayman Hariri
Yang Huiyan
Albert Von Thurn Und
Taxis




No comments:
Post a Comment