Wednesday, 6 June 2012

Tweet kutoka kampuni ya Asus iliozua Utata


 Ni ujumbe wa twita, uliozua mijadala kwenye mitandao ya intaneti kwa kushutumiwa kuwa unamdhalilisha mwanamke. Kampuni ya Electronics Asus iliufuta ujumbe wake huo ulioambatanishwa na picha inayomuonyesha mwanamke akielezea bidhaa mpya ya kampuni hiyo mara tu baada malalamiko kuanza.
Ni picha iliopigwa kwa kuuchukua upande wa nyuma ya mwili wa mrembo huyo ikiambatana na ujumbe unaosema “ picha ya nyuma ni nzuri sana,  kama ilivyo Transformer AIO”
Posti hiyo ilipotea kwa haraka sana, ila walichelewa kwani ilishadakwa na watu kuanza kuichangia na wenzao, na kusambaa kwa kasi kwenye mitandao mingine na  malalamiko na shutuma kuanza kuelekezwa kwa kampuni hiyo.hata hivyo kampuni ya Asus iliomba radhi kwa tukio lake hilo, na kuahidi kuchukua hatua ambazo zitahakikisha kosa hilo halitojitokeza tena
Utamadani wa kuwatumia wanawake warembo kwenye maonyesho ya bidhaa, umekuwa ni utaratibu wa wakawaida kwa makampuni ya elektroniki duniani. Ila tahadhari itumike, na kwa uangalifu wa karibu zaidi, aliongezea Bi susan Friedmann mtaalamu wa maswala ya ya biashara kwa kusema “ nilazima uzingatie unapofanya maonyesho kama haya, kinachoweza kukufunga Paducah yaweza kuwa sawa na Tokyo”

No comments:

Post a Comment