Thursday, 24 May 2012


Pangilia maisha yako ya kazi
Kama shuhuli zako za kazini zinakuacha ukiwa na mvutano wa mawazo, au unajihisi ni kama uliyezingirwa na kuzidiwa na mambo, tambua umefika muda wa kutulia, na kupangilia mambo yako.Kwanza hakikisha unawasili kazini japo dakika tano kabla ya muda unaotakiwa kuripoti kazini, utaratibu huu utakupa muda wa kupanga majukumu yako ya siku hiyo, na kujituliza kisaikolojia vile vile.
Pili tenga nafasi ya kutosha ya kufanyia kazi, kwa kutoa vitu vilivyozagaa mezani, au eneo lako la kufanyia kazi kwa ujumle, pamoja na kufuta email za zamani ambazo hazina umuhimu, pitia email za kwenye scam japo kwa juuu huwezi jua panaweza kuwa na ujumbe wa muhimu kasha ndio uzifute fanya hivi mara kwa mara ili zisiwe nyingi ukajikuta huwezi kuzithibiti ipasavyo. Kasha andaa orodha ya mambo ambayo utahitajika kufanya kwa siku hiyo, fanya hivyo kwa kuzingatia kipaunmbele. Ukiweza jaribu kuanza na kazi ngumu, ilikuondoa mzigo wa mawazo kichwani mwako.


Vaa vazi litakalo ibua mudi yako
Ilhali wengine wetu tunalazamika kuvaa uniform za kazini au mpangilio Fulani wa nguo unaokubalika kazini, kama una uhuru wa kutosha yaani hamjawekewa vikwazo vya nguo aina gani za kuvaa, chagua nguo au vikolombwezo  vitakavyo kupa uchangamfu, kama utavaa mikufu itakayokuletea kumbukumbu nzuri, begi zuri lenye rangi nzuri litakalo angazia siku yako, au vazi ambalo litakokuza kujiamini kwako, au hata nguo yako ya ndani, vaa vazi ambalo litaangazia siku yako na kukufanya uwe mwenye furaha
Badilisha  Mpangilio wako wa kazi
Kuwa mienendo yako sio lazima kila mara uwe unafata utaratibu ule ule, katika maisha yako ya kazi ya kila siku, kufata utaratibu huo huo kila siku itakufanya ujisikie ni mwenye kukosa mizuka. Kwa hiyo jaribu kitu kipya au utaritibu mpya kila inapowezekana kwa namna yoyote unavyoweza.Fanya kazi za kila siku katika mpangilio mwingine, kuongea na mtu ambaye hukuwahi zungumza naye hapo kabla, au  hata kutumia usafiri wa aina tofauti, kama baiskeli. Kama umeshindwa kabisa kubadilisha mpangilio wako wa kazi basi , jaribu kitu kizuri, cha kusisimua na tofauti wakati wa chakula cha mchana  aua wakati wa mapumziko.


Ongeza nuru mezani kwako


Utafiti unaonyesha kuwa wafanyakazi waliochukua muda kungarisha au kuweka athari kwenye meza au eneo lao la kazi, basi wanauwezekano mkubwa wa  kuwa na furaha asilimia 40 ya furaha kulinganisha na wenzao. Inawezekana ukakosa idhini au mamlaka ya kuremba eneo lako la kazi, ila kama unaweza basi pangilia ofisi yako au eneo lako la kazi, kwa kununua vitu binafsi, kama vya steshonari, picha ya sherehe Fulani hivi, kalenda ya kuchekesha au kitu cha sanaa, au hata mmea, mazingira mazuri yenye kuvutia ni lazima yata kuchan

Changamka kazini
Kama kazi yako inakuboa, jaribu kujichangamsha, kwa kujipa viji zoezi kipindi cha mapumziko ya chakula cha mchana.mazoezi ni mazuri kwa kukuchangamsha, huongeza kujiamini kwako, na kupoteza mvutano wa mawazo, na vile vile inapelekea ubongo kuachia aina Fulani ya kemikali iitwayo endorphins na anandamide ambazo zaweza kukuchamngamsha na kukuacha mwenye kujisikia furaha, na huru. Kama kuna bafu, basi pata shawa, au tembea tembea kama ni madukani kuchangamsha mapigo yako ya moyo, na hutokuwa na  haja ya kuoga.
Tafuna tafuna vitafunwa
Je unasiku ngumu mbeleni? basi hakikisha umepaka vitu vizuri kwenye begi lako unapoenda kazini, vitakuongezea nguvu, vitu kama vya sukari sukari, na kukuchangamsha vile vile.baadhi ya virutubisho kwenye chakula vya weza kuchangia namna ambavyo unajisikia, vyakula kama ndizi, vyakula vya nafaka.
Kuwa positive/chanya na mchangamfu kwa wenzako.
Bila kujali namna ambavyo unajisikia, jaribu kuwa mchangafu kwa wenzako, hata wale ambao wanakukera  na kukuchefua mno.Jaribu kusuluhisha  migogoro, epusha umbea, na mtendee wema kila mmoja pasi na kubagua, utafiti unaonyesha kitendo cha kutabasamu yaweza kukufanya uwe na furaha zaidi, kwa hio jaribu kulazimisha tabasamu
Ridhika kwa kuwa unakazi
Kama unaona kuwa aina ya kazi unayofanya, si unaoipenda, jilazimishe kufanya vyema.yaweza kuwa ya moja kwa moja, ila kwenda kila siku, pasi na wewe kuona sababu ya msingi kwenda hapo si muda mrefu itakukwaza. jaribu kujitengenezea mitazamo chanya, kuhusu kazi hiyo, kwa kuwa saidia watu wengine kama unaweza.


No comments:

Post a Comment