Tuesday, 22 May 2012

Kwa nini viatu Virefu


Wanawake walio wengi katika kipindi cha maisha yao huvaa viatu virefu, huvaliwa kuongeza urembo, huifanya miguu, ivutie, kuonekana mirefu miembamba na yenye mvuto.na upande mwingine wanaume huvutiwa na wanawake wanapokuwa wamevaa viatu virefu
         Kwa wengine wetu viatu virefu ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku, huvaa tuendapo ofisini, tunapokuwa kwenye matembezi ya mwisho ya wiki, mitoko ya jioni, au katika shuhuli maalum, hayo yote ni kwa ajili tuu ya kuonekana warembo. Kwa nini usijihusishe na viatu ambavyo ambavyo vitavuka matetegemeo yako
   Miaka iliyopita nilikuwa na viatu virefu vizuri na vibaya. kuna viatu virefu vya aina tofatuti madukani, virefu sana, vyembamba chini ya nchi mbili, na vyenye unene wa nchi 0.4.
Kuna faida nyingi ya kuvaa aina hii ya viatu, inaulazimisha mwili kuweza kuzunguka, inafanya muonekana wa makalio na matiti kuvutia, muonekano wa mwanamke wa kisasa.
Hufanya  visigino kuonekana vidogo, hufanya mifupa inayotengeneza unyayo kuwa mirefu kuinuka na yenye kuleta maana zaidi. hupelekea mkao(posture) ya mvaaji kutulia kitu ambacho husaidi uti wa mgongo.
Nina urefu wa nchi 5’5” sio mrefu wala mrefu, nipo katikati.ila tayari ninayo miguu mirefu, ninapo vivaa viatu urefu wangu huongezeka hadi kufikia 5’7”.Viatu vyangu virefu huwa kwenye maboksi yake kabatini.huwa navaa, kwa mitoko ya usiku, maharusi na wakati mwingine ili tuu niwe na muonekano wa  miguu mirefu.
Style yangu kifashen hubadilika mara kwa mara hujikuta na vaa viatu vye muonekano tofauti kwa madhumuni tofauti, hupenda sehemu ya chini ya miguu yangu ionekane hasa pale, ninapovaa nguo simple, viatu  vyangu hunitoa moja kwa moja na kunijengea kujiamini.

Najua kuwa mara kadhaa vaitu virefu huu miza miguu, hata mimi imewahi kunitokea, Hizi ndio nyenzo zangu ambazo hutumia, na pengine itapelekea viatu vyako hivyo vya gharama kukunufaisha
Nunua kiatu cha saizi yako: bila shaka hii inaonekana kuwa ni kitu cha kawaida, ila lini ilikuwa mara ya mwisho kwako kwenda dukani kwa ajili ya kupima urefu wa miguu yako.Wataalamu wanaamini kuwa miguu huongezeka urefu kadri siku zainavyokwenda, na ujauzito huweza pelekea urefu wa unyayo wa mguu kuongezeka vile vile. ndio maana ni muhimu kupima urefu wa miguu yako, kila unapo enda kununua viatu.hakikisha hakuna nafasi iliobakia yenye urefu sawa na kidole gumba kati ya kidole chako kirefu cha miguuni na mwisho wa kiatu, kwa viatu virefu ni muhimu kufanya hivi ili uweze kustarehe pale utapo vivaa.
Vaa vyenye  uduara
Tumebahatika kwa kuwa viatu vya duara huwa havitoki kwenye fasheni ukilinganisha na vilivyo chongeka mbele, vilivyo chongeka vyaweza kukupeleka kupindisha kidole chako kirefu kwa ndani, chanzo cha maumivu ya vidole, na hata kupata sugu vidoleni, ilhali viatu vyenye uduara mishoni hukupa nafasi ya kunyoosha vidole vyako.iwapo huwezi kuachana  kabisa na viatu virefu basi basi kuwa na vya uduara ili kubadilisha pale itapokulazimu.
Tambua unene wa kiatu.
Wakati mwinginie vidole sio tatizo, zingatia unene wa kiatu.viatu vingi vya fasheni huja katika unene wa kawaida, ila kama una nyayo nene, unene wa kawaida utakupa shida. Unapokutana na kiatu kinachokuvutia, angalia kama kuna kingine chake ambacho unene wake unaendana na wewe, kama sivyo basi mafundi viatu huweza kuvinyoosha na na kuongeza komfotability.
Vijaze nyama.
Baada ya kuzingatia kuwa viatu hivyo havikubani, sasa ni wakati wa kuangalia kama vina nyama kutosha.mara nyingi visigino na unyayo kwa ujumla huuma kwa sababu ya maumivu yatokanayo na kitako cha viatu, jaribu kutafuta namna ya kupunguza maumivu hayo

 Kiatu mbadala

Kuvaa viatu virefu kwa muda mrefu, huweza kukufanya ujisikie kama nyayo zako zimeinuka.Ili kuendeleza comfort , jenga utaratibu wa kuvaa viatu vya kawadia. Ingawa viatu virefu, hukuza urefu wa miguu yako, havina umuhimu sana pale unapovaa suruali, kwa hio upe unyayo wako mapumziko.
Tunnza nyayo za miguu yako.
Hakuna kinacho haribu muonekano wa viatu virefu kama unyayo usio na mvuto, kama unamalengo ya kuonesha vikuku vya miguuni, basi wekeza kwenye pedicure angalau kila wiki.
Inachukua muda kuzoea viatu virefu , ila kuwa na viatu vyako vya kawaida  iwapo lolote likijitokeza, tembea na plasta huwezi jua michubuko yaweza kujitokeza wakati gani.
Kwa kuhitimisha, tafadhali tunza miguu yako, viatu virefu vinapendeza na kila mtu anavipenda
“sijui ni nani aliyegundua viatu ila kila mwanamke ana deni kwake”marilyn Monroe


Makala zingine


http://kipepe-sikika.blogspot.co.uk/2012/05/sababu-halisi-inayokufanya-uwena-uchovu.html

No comments:

Post a Comment